ZABUNI BARABARA ZA JUU KUTANGAZWA MWEZI UJAO


Zabuni  ya ujenzi wa barabara za juu jijini Dar es Salaam inatarajiwa kutangazwa mwezi ujao.

Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli alitoa taarifa hiyo wakati wa hafla ambayo serikali ya Japan ilitia saini mkataba wa kusaidia serikali fedha za ununuzi wa magari ya kubebea wagonjwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na mashine ya kukamulia mafuta ya alizeti wilayani Chato.
Ingawa Magufuli hakuzungumzia undani wa mchakato huo,  alisema taratibu zinaendela vizuri kwa ajili ya ujenzi huo.
“Tunatarajia kutangaza tenda ya ujenzi wa barabara za juu mapema mwezi wa tatu mwaka huu,”  alisema Magufuli.
Ujenzi wa barabara za juu jijini Dar es Salaam, ulifikwa na serikali ikiwa ni hatua mojawapo ya kupunguza tatizo la msongamano wa magari, unaosababisha foleni kubwa na adha kwa wananchi.
Barabara za juu zinatarajiwa kujengwa katika eneo la Tazara na  eneo la Ubungo.

No comments: