Wakazi wawili wa kata ya Kigongoi wilayani Mkinga, wamekufa papo
hapo baada ya kufukiwa na kifusi cha udongo walipokuwa wakichimba madini aina
ya vito.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Juma Ndaki
alibainisha hayo wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu matukio
mbalimbali mkoani humo.
Aliwataja waliokufa ni Nyange Mussa (21) ambaye ni
mkazi wa kitongoji cha Hemsambia na Kagembe Shabani (19) wa kitongoji cha
Shashui kata ya Kigongoi wilayani Mkinga.
“Ajali hii iliyosababisha vifo ilitokea juzi kwenye eneo la
mgodi unaomilikiwa na Charles Kifunta wakati wahusika walipokuwa ndani ya mgodi
ghafla walishukiwa na gema la udongo (kifusi) na kufa papo hapo”,
alisema.
Kamanda Ndaki (pichani) alisema katika tukio hilo, Alex Remo (24)
amejeruhiwa. Hata hivyo alisema hali ya afya yake kwa sasa inaendelea
vizuri.
Alisema hakuna mtu aliyekamatwa kuhusu tukio hilo, ingawa
uchunguzi wa polisi unaendelea.
No comments:
Post a Comment