UPELELEZI KESI YA WAFUASI WA CUF BADO KUKAMILIKA


Upelelezi wa kesi ya kutotii amri halali ya polisi na kufanya mkusanyiko usio halali inayowakabili wafuasi 30 wa Chama cha Wananchi (CUF) haujakamilika.

Wakili wa Serikali Joseph Maugo alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Emilius Mchauru wakati kesi hiyo ilipotajwa.
Hakimu Mchauru aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 26, mwaka huu itakapotajwa kwa ajili ya kuangalia kama upelelezi umekamilika.
Washitakiwa wanadaiwa  Januari 27, mwaka huu , wilaya ya Temeke, washitakiwa wote walikula njama ya kufanya kitendo cha uhalifu.
Katika mashitaka yanayowakabili mshitakiwa wa kwanza hadi wa 28, wanadaiwa siku hiyo katika ofisi za CUF, karibu na Hospitali ya Temeke, bila halali walifanya mkusanyiko kwa nia ya kufanya maandamano yasiyo halali kwenda viwanja vya Mbagala Zakhem.
Aidha, washitakiwa wanadaiwa siku hiyo katika eneo la Mtoni Mtongani, Temeke, waligoma bila kujali tangazo halali lililotolewa na Polisi  la kuzuia kukusanyika na kuandamana isivyo halali.
Kwa mujibu wa hati ya mashitaka, washitakiwa hao ni Shabani Ngurangwa, Shabani Tano au Kasakwa, Shabani Polomo, Juma Mattar, Mohammed Kirungi , Athumani Ngumwai, Shaweji Mohamed, Abdul Juma ,Hassan Saidi , Hemed Joho , Mohamed Mbarouk  na Issa Hassani.
Wengine ni Allan Ally, Kaisi Kaisi , Abdina Abdina, Allawi Msenga, Mohamed Mtutuma, Salehe Ally, Abdi Hatibu, Bakari Malija, Abdallah Ally , Said Mohamed, Salimu Mwafisi, Saleh Rashid, Abdallah Said, Rehema Kawambwa, Salma Ndewa, Athumani Said, Dickson Leason  na Nurdin Msati.

No comments: