Taasisi
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imesema kuwa haikurupuki katika
kuwashughulikia na kuwafikisha mahakamani viongozi wanaotuhumiwa kujipatia
fedha kutoka kwenye akaunti ya Tegeta Escrow na kwamba ushahidi pekee ndiyo
itakaofanya kuwafikisha mahakamani watuhumiwa.
Akizungumza
mara baada ya kuzindua jengo la ofisi ya mkoa la Taasisi hiyo mjini Kigoma
juzi, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hoseah alisema hakuna atakayeachwa
katika sakata hilo iwapo ushahidi utathibitisha pasi na shaka kwamba alihusika.
Alisema
uchunguzi dhidi ya viongozi na watu mbalimbali waliohusina na uchotaji wa fedha
hizo unaendelea na kwamba ushahidi utakapokamilika kila mmoja atapata kile
anachostahili bila kumuonea mtu.
“Hatutaki
kukurupuka katika kushughulikia watuhumiwa wa sakata la Escrow na muhimu ni
ushahidi ambao utawatia hatiani watuhumiwa, ni aibu kwangu kumfikisha mtuhumiwa
mahakamani na mwisho wake siku ushahidi hautoshi na mtuhumiwa kuachiwa huru,”
alisema Dk Hoseah.
Aliwataka
wananchi kuwa na imani na chombo hicho katika kushughulikia suala hilo na
kwamba haki itatendeka kwa kuwashughulikia watuhumiwa wote kwa haki badala ya
kufuata kelele zinazopigwa kwamba hawafanyi kitu au kuwashughulikia watuhumiwa
wakubwa.
Tangu
kuibuka kwa sakata la kuchotwa kwa fedha katika Akaunti ya Tegeta Escrow
iliyokuwa imefunguliwa katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) baada ya kuwepo kwa
mgogoro wa kibiashara baina ya Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) na kampuni ya
kufua umeme ya IPTL, hatua kadhaa zimechukuliwa na Serikali.
Hizo
ni pamoja na kuvunjwa kwa Bodi ya Wakurugenzi Tanesco, kutenguliwa kwa Uwaziri
wa Dk Anna Tibaijuka aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
lakini pia Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alijiuzulu
mwishoni mwa mwaka jana, kama ilivyokuwa kwa Waziri wa Nishati na Madini,
Profesa Sospeter Muhongo aliyejiuzulu mwezi uliopita.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati, Eliakim Maswi amesimamishwa ili kupisha uchunguzi wa
tuhuma dhidi yake juu ya ushiriki wake katika sakata hilo lililoteka mkutano wa
16 na 17 wa Bunge ambao uliibuka na maazimio manane, yakiwemo ya kuwawajibisha
waliotajwa kuhusika kwa namba moja ama nyingine uchotwaji wa karibu sh bilioni
300 katika akaunti ya Escrow.
No comments:
Post a Comment