Katika
hali isiyokuwa ya kawaida, mkazi wa mjini Namanyere wilayani hapa mkoa wa
Rukwa, Gilbert Paul (37) aliyejiandalia maziko yake miaka 14 iliyopita, bado yu
hai.
Kwa
sasa mtu huyo ameanza maandalizi ya
kuchimba na kujenga kaburi la gharama, ikiwa ni pamoja na kununua jeneza.
Paul,
baba ya mtoto mmoja na mchoraji maarufu mjini Namanyere aliyehitimu Kidato cha
Nne 2001 katika Shule ya Sekondari
Nkasi, anasema anafanya hivyo kwa kuwa ana amani maisha ya duniani yana ukomo
wake na ni ya kupita tu.
Aliyasema
hayo juzi, akithibitisha kujichongea msalaba mkubwa na kuutundika kwenye paa la kibanda chake anamofanyia kazi zake katika Mtaa wa Sasala.
Msalaba
huo mweupe mkubwa,
umeandikwa tarehe aliyozaliwa ya
Desemba 24, 1977, lakini katika tarehe ya kufa, ameweka alama ya kiulizo. Msalaba huo unaonekana
waziwazi, kiasi cha wageni wanaopita eneo hilo, kudhani ni nyumba ya ibada.
Paul alisisitiza kuwa msalaba huo uliofikisha
miaka 14 sasa, ndio utakaosimikwa
katika kaburi lake,
ambalo anatarajia kulichimba na
kulijengea, akikadiria litamgharimu Sh milioni moja, sawa na gharama ya jeneza
alilotarajia kulinunua.
“Nilipotafuta
mafundi wanitengenezee msalaba huu, wote waligoma
wakidai ni uchuro na hawajawahi kusikia wala
kuona mtu akijifanyia maandalizi
yake ya maziko akiwa bado anaishi .
“Mama alilia sana walipomtaarifu, akidai katika ukoo wa baba yangu na wa kwake
hakuna aliyewahi kufanya hivyo
…Baba alifariki nikiwa na miaka saba, mwanzoni watu
walidhani nina tatizo la akili na wengine waliamini nimeathirika kwa
Ukimwi hivyo nimekata tamaa ya kuishi, lakini sivyo…“ anasema.
Alieleza
kuwa katika maisha yake yote, hakuwahi kuwa na rafiki wa kike mjini
humo kutokana na kujitengenezea msalaba huo, unaomfanya wamuogope sana, hadi kuona kuna ulazima wa yeye
kwenda kijiji cha mbali na hapo .
“Nilichumbia
na kuoa chapuchapu nikihofia mke wangu mtarajiwa akibaini nimejitengenezea
msalaba hatanikubali,“ alieleza.
Mke
wa Paul, Paskaria Salvatory (25) akizungumzia tukio hilo, anasema kama
angefahamu, kamwe asingekubali kuolewa naye.
“Si
kawaida mtu kujitayarishia maziko yake mwenyewe akiwa hai. Nilibaini mwezi mmoja baada ya kuolewa, kwa kweli
nilishituka sana, pia wanawake
wenzangu walikuwa wakinibeza na
kuniita kwa majina ya kuudhi, lakini
sasa nimezoea na nimezaa naye mtoto mmoja mwenye umri wa miaka miwili.
Mume wangu ana akili timamu, ni mwenye
huruma na anayejali familia“, alibainisha.
No comments:
Post a Comment