Wakala
wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), unategemea kuanza rasmi mkakati wa
kuwasajili na kuwapa vyeti vya kuzaliwa wanafunzi wa shule za msingi za
Manispaa ya Kinondoni na mpango huo utatekelezwa katika takribani
shule 140 zenye wanafunzi wapatao 155,944.
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kitengo cha mawasiliano
cha wakala huyo, lengo la usajili huo katika awamu hiyo ni kusajili wanafunzi
20,000.
Ilisema
kuzinduliwa kwa mkakati huo katika Manispaa ya Kinondoni ni muendelezo wa
mkakati mkuu uliozinduliwa Aprili, mwaka jana unaowawezesha wanafunzi wa Shule
za Msingi na Sekondari kusajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa katika shule
wanazosoma.
Taarifa
ilisema baada ya mwalimu kuwatangazia wanafunzi na wazazi kuhusu huduma hiyo
kupatikana shuleni atagawa fomu za maombi kwa wanaohitaji, kuhakiki fomu
zilizojazwa, kuzikusanya na kuziwasilisha
RITA kwa ajili ya kuhakiki na kuandaliwa vyeti.
Tayari
mkakati huo umeshaanza kutekelezwa katika Manispaa ya Ilala jijini Dar es
Salaam na umeshafanyika katika shule 105 za msingi na 96 za sekondari za
Manispaa ya Ilala na kuonesha mafanikio ambapo zaidi ya wanafunzi 16,000
wamesajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa.
No comments:
Post a Comment