Mfanyabiashara
mashuhuri, Marijan Abubakar maarufu kama Papaa Msofe (50) anayekabiliwa na kesi
ya mauaji, ameshindwa kufika mahakamani kwa kuwa anaumwa.
Kesi
hiyo ilitajwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu lakini Wakili wa Serikali
Hellen Moshi alidai bado upelelezi haujakamilika na kwamba Papaa Msofe
hakufika mahakamani, kwa kuwa wamepata
taarifa kuwa anaumwa.
Hakimu
Mkazi Hellen Riwa aliahirisha kesi hiyo hadi Machi 5, mwaka huu itakapotajwa
tena kwa ajili ya kuangalia kama upelelezi umekamilika.
Msofe
ambaye kwa mara ya kwanza alifikishwa mahakamani hapo Agosti 10, mwaka 2012
anadaiwa Novemba 6, mwaka 2011 katika eneo la Magomeni Mapipa, yeye na mwenzake
Makongoro Nyerere, kwa kukusudia walimuua Onesphory Kitoli.
Washitakiwa
wanaendelea kusota rumande kwa kuwa kesi inayowakabili kisheria haina dhamana.
No comments:
Post a Comment