PADRE SANGU APONGEZWA KWA KUTEULIWA ASKOFU


Rais Jakaya  Kikwete ametuma salamu za pongezi kwa uteuzi uliofanywa na Baba Mtakatifu, Papa Francis wa Padre Liberatus Sangu wa Jimbo la Sumbawanga kuwa askofu wa jimbo Katoliki la Shinyanga.

Alituma salaam hizo kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na Askofu wa Jimbo Katoliki la Iringa, Mhashamu Baba Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa na kuomba salaam hizo afikishiwe Padre Sangu.
Askofu Mteule Liberatus Sangu aliyekuwa Ofisa katika Idara ya Uenezaji wa Injili kwa Mataifa katika Makao Makuu ya Kanisa Katoliki, Vatican, anatarajiwa kupewa Daraja la Uaskofu na kusimikwa rasmi kuwa Askofu wa Jimbo la Shinyanga Aprili 12 mwaka huu.
Alisema, “Hii inadhihirisha wazi kutambuliwa kwa mchango mkubwa wa Padre Sangu katika kuwatumikia kikamilifu Kondoo wa Bwana hususan kupitia Idara nyeti ya Uenezaji wa Injili kwa Mataifa aliyokuwa akiitumikia akiwa Vatican ambako ndiyo Makao Makuu ya Kanisa Katoliki Duniani.”

No comments: