Bodi ya wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa
Huduma ya Nishati na Maji (EWURA) imepitisha maombi ya Shirika la Maendeleo ya
Petroli Tanzania (TPDC) kuhusu kanuni za tozo za huduma ya kuchakata na
kusafirisha gesi asilia.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini, Mkurugenzi Mkuu EWURA, Felix Ngamlagosi
alisema TPDC iliiomba Ewura kuidhinisha vipengele vya kanuni ya
kurekebisha tozo za kuchakata na
kusafirisha gesi asilia itumike kwa miaka 20 hadi mwaka 2034, tozo kwa huduma
ya kuchakata na kusafirisha gesi asilia iwe katika dola za Marekani.
Pia waliomba faida kwenye mtaji ya asilimia 18 na muundo wa mtaji wa
asilimia 50 mkopo na asilimia 50 fedha za TPDC na mwezi Septemba kila mwaka wa
tatu utakuwa ni mwezi ambao marekebisho ya tozo kwa miaka mitatu inayofuata
yatawasilishwa kwa EWURA.
Alisema bodi ya EWURA ilijadili
ombi la TPDC na kufikia maamuzi ya kipindi kifupi cha miezi mitatu ambacho TPDC
itakitumia kukamilisha ujenzi na kuwasilisha gharama halisi ambayo EWURA
iliyahoji.
Aliongeza kuwa maamuzi yaliyotolewa na EWURA ni kanuni ya kukokotoa tozo za kuchakata na kusafirisha gesi asilia
iliyoombwa ilirekebishwe na kupitishwa ili itumike kwa miaka 20 kuanzia mwezi
Aprili mwaka huu na kurekebishwa kila baada ya miaka mitano.
Pia gharama za mradi wa bomba la kusafirisha gesi asili kutoka Mtwara
hadi Dar es Salaam zilizopitishwa ni
sawa na dola za Marekani milioni 1,331,51 ambapo gharama hizi zitabaki hivyo
hadi mwezi Juni hadi gharama halisi za mradi zitakapojulikana na kufungwa.
Alisema maamuzi mengine ni gharama za uendeshaji zitakuwa sawa na dola
za Marekani milioni 241.58 kwa mwaka na muundo wa mtaji kwa ajili ya mradi wa
bomba la gesi asilia Mtwara hadi Dar es Salaam litagharamiwa kwa mkopo wa kiasi
cha asilimia 75 na mtaji wa TPDC.
Aidha mradi wa miundombinu ya bomba na mitambo ya kuchakata gesi asilia
utatekelezwa kipindi cha miaka 20 kutoka
tarehe ya uzinduzi wake na tozo ya
kuchakata gesi italipwa kwa Shilingi ya
Tanzania kwa kiasi sawa na jumla ya dola za Marekani 2.14 kwa uniti ambapo tozo
ya kuchakata gesi itakuwa dola za Marekani 0.95 kwa uniti na tozo ya kusafirisha gesi itakuwa dola za
Marekani 1.19 kwa uniti.
Pamoja na maamuzi hayo pia EWURA imewataka TPDC kutimiza masharti ya
kuzingatia kanuni za ushindani kama zilivyoainishwa katika sheria ya manunuzi
ya Umma ya mwaka 2011 na kuiarifu Ewura kila watakapofanya manunuzi ya thamani
yanayozidi dola za Marekani milioni tano.
No comments:
Post a Comment