Mamia
ya wananchi wakiongozwa na Rais wa Zanzibar,
Dk Ali Mohamed Shein walihudhuria maziko ya aliyekuwa mnadhimu wa Chama
Cha Mapinduzi Baraza la Wawakilishi na Mwakilishi wa jimbo la Magomeni, Salmin
Awadh Salmin kijijini kwao Kiungoni Makunduchi mkoa wa kusini Unguja.
Awadh
alifariki ghafla juzi wakati alipokuwa katika ofisi kuu ya CCM Kisiwandui mjini
hapa ambapo alikuwa akihudhuria vikao mbalimbali vya Chama Cha Mapinduzi.
Mwili
wa marehemu Awadh uliagwa na viongozi mbalimbali wa serikali na vyama vya siasa wakiongozwa na Makamu wa
Pili wa Rais, Balozi Seif Ali Iddi katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi
Chukwani Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.
Akitoa
salamu kwa waombelezaji waliohudhuria msiba huo katika jengo la Baraza la
Wawakilishi, shehe kutoka Kamisheni ya Wakfu na mali za amana, Thabit Norman
Jongo alisema ni msiba mkubwa kwa taifa na familia ya marehemu kwa ujumla.
Hata
hivyo, alisema msiba huo unawakumbusha waumini na wananchi kwamba kila nafsi
itaonja umauti, kwa hiyo njia pekee ya kujiweka salama katika safari ya mwisho,
kwa kila binadamu ni kufanya ibada.
Mwili
wa marehemu Awadh uliswaliwa katika Msikiti wa Masjid Noor ambapo safari ya
mwisho ya marehemu ilianzia hadi Makunduchi kilomita 54 kutoka mjini.
No comments:
Post a Comment