Dereva
bodaboda Ismail Lucas (16), mkazi wa Kwa Mathias wilayani Kibaha mkoani Pwani,
anatuhumiwa kumlawiti mtoto ambaye ni
mwanafunzi wa Chekechea.
Mama wa mtoto huyo (jina limehifadhiwa) alisema
kuwa kutokana na tukio hilo, mwanawe (jina limehifadhiwa) alijeruhiwa vibaya.
Alisema kuwa tukio hilo lilitokea saa 3:00
asubuhi eneo la Tanita wakati mtoto huyo alipokuwa akitokea dukani akiwa
ameongozana na mwenzake, mtoto wa mama yake mkubwa mwenye umri wa miaka saba,
ambaye alikuwa amewaagiza mkate.
“Mama yake mkubwa aliwatuma dukani Kwa Mrisho
ambapo walinunua mkate na walipokuwa wakirudi, walikutana na mtuhumiwa ambaye
alimrubuni mwanangu kuwa ameangusha chenji
iliyorudi dukani hivyo aende akampe,” alisema.
Alisema kuwa mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa na
pikipiki, alimchukua na kumpeleka kwenye vichaka ambavyo viko jirani na
barabara huku mwenzake akiwa analia kuomba msaada.
“Alikwenda naye huko vichakani na kumfanyia
vitendo hivyo, mama mmoja Clara Edwin
alikuwa akipita hapo na alipomwona mtoto aliyekuwa akilia alimwuliza imekuwaje, akamwambia mwenzangu
kachukuliwa na mtu asiyemfahamu na kuelekea eneo la tukio, ndipo mtuhumiwa
alipokimbia na kuacha pikipiki yake,” alisema.
Alisema kuwa yeye hakuwepo nyumbani, lakini
alijulishwa kuwa mwanawe kafanyiwa mchezo huo, ambapo alipomwona mwanawe akiwa
kwenye hali ile, alipoteza fahamu.
“Majirani walinisaidia baada ya muda nilizinduka
na kumpeleka mtoto kituo cha Polisi cha Kwa Mathias na baadaye Hospitali ya
Mkoa ya Tumbi kwa ajili ya matibabu ambapo hadi sasa anaendelea vizuri baada ya
kupatiwa matibabu,” alisema.
Kwa upande wake, Clara ambaye ndiye aliyemuokoa
mtoto huyo, alisema yeye baada ya kwenda kule vichakani mtuhumiwa alikimbia
kusikojulikana na wasamaria waliipeleka
pikipiki hiyo kwenye kijiwe anachofanyia kazi na ndipo walipobaini kuwa ni ya
Lucas.
“Wasamaria wema wakishirikiana na madereva
bodaboda wenzake, walifika nyumbani kwao na kumkuta mlezi wake ambapo
walimwambia asimruhusu kuondoka hadi polisi watakapofika, ambapo walimchukua na
kumpeleka kituoni,” alisema.
Akithibitisha kutokea tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Ulrich Matei
(pichani juu) alisema mtuhumiwa huyo anashikiliwa na atafikishwa mahakamani mara upelelezi
utakapokamilika.
No comments:
Post a Comment