Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Nzega
mkoani Tabora imemhukumu kifungo cha maisha
Kashindje Shija (50), baada ya kupatikana na kosa la kumbaka mtoto
mwenye umri wa miaka mitano.
Akisoma hukumu hiyo mwishoni mwa wiki, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Nzega
Joseph Ngomero, alisema kuwa, kutokana na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo,
amelazimika kutoa hukumu hiyo ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaokusudia kufanya
vitendo kama hivyo.
Hakimu Ngomero aliongeza kwa kusema kuwa,
kutokana na kitendo cha kinyama alichokifanya Shija cha kumbaka mtoto mwenye
umri wa miaka 5, mahakama hiyo imelazimika kumhukumu kifungo cha maisha jela.
Awali Mwendesha Mashitaka wa Serikali wilayani
Nzega Melito Ukongoji aliiambia mahakama hiyo kuwa, mnamo Mei 19, 2014
katika Kijiji cha Kidete wilayani
Nzega saa 8 mchana, Shija alifumaniwa
chini ya mti wa mwembe akiwa anambaka mtoto huyo.
Aidha Melito aliongeza kuwa kutokana na kitendo
alichokifanya mtuhumiwa
kilimsababishia mtoto huyo maumivu makali
katika mwili wake pamoja na kutoka damu
nyingi.
Mwendesha Mashitaka huyo, aliiomba mahakama
hiyo kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama
hizo kutokana na kitendo kilichofanywa
na mtuhumiwa cha kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka 5.
Kabla ya hukumu hiyo kutolewa, mahakama hiyo
ilitoa nafasi ya utetezi kwa mtuhumiwa ambapo aliiomba mahakama hiyo
kumpunguzia adhabu kutokana na kuwa mwathirika wa virusi vya Ukimwi.
No comments:
Post a Comment