MVUVI AJERUHIWA NA KIBOKO, WAWILI WAPONEA CHUPUCHUPU


Shukurani Kando (34) ambaye ni mvuvi na mkazi kitongoji cha Kalumo kijiji cha Nambubi, Kata ya Kisorya amejeruhiwa kwa kung’atwa na kiboko na wengine wawili kunusurika wakati wakivua katika Ziwa Victoria wilayani Bunda, Mkoa wa Mara. 
Kwa mujibu wa diwani wa kata hiyo, Misana Jigwila tukio hilo ni la juzi saa 1:00 asubuhi ambapo alisema kiboko huyo alitokea ghafla wakati wavuvi hao wakiendelea na uvuvi. Alisema walionusurika waliogelea hadi nchi kavu.  
“Walikuwa watatu, sasa wakati wakiendelea kuvua ghafla kiboko huyo alitokea na kuanza kuwashambulia na kumjeruhi huyo mmoja, wengine wawili walinusurika baada ya kuogelea hadi nchi kavu,” alisema. 
Alisema majeruhi alipelekwa hospitali ya wilaya ya Nansio kutokana na kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili wake na hali yake si nzuri.

No comments: