WABUNIFU WA MAJENGO KUKUTANA LEO DAR


Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili,  Ali Hassan Mwinyi, leo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano wa 22 wa wataalamu wa wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi utakaofanyika kwa siku moja jijini Dar es Salaam.
Mbali na Mwinyi, alisema pia atakuwemo Waziri wa Ujenzi Dk John Magufuli na wanafunzi kutoka shule mbalimbali za sekondari.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Msajili wa Bodi ya Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB), Jehad Abdallah Jehad, alisema mkutano huo utakaohudhuriwa na washiriki wapatao 400, mada kuu itakuwa sheria ya manunuzi namba 7 ya mwaka 2011 na athari zake katika mazingira ya ujenzi.
Mwenyekiti wa AQRB, Ambwene Mwakyusa alisema mategemeo yao ya baadaye katika mashindano hayo ni kuendelea kuhamasisha wanafunzi kupenda masomo ya sayansi hususani taaluma za ubunifu na ukadiriaji majenzi ili kukidhi pengo la upungufu uliopo ambapo hadi kufika mwaka 2025 wanataka kuwa na wataalamu wa aina hiyo walau 6,500 kutoka 1,000 waliopo sasa.

No comments: