MICROSOFT WAZINDUA SIMU ZA TEKNOLOJIA YA KISASA



Kampuni ya Microsoft imezindua simu tatu aina ya Nokia Lumia zilizounganishwa na  mfumo wa kisasa wa teknolojia ya uendeshaji wa simu wa Windows Phone 8.1.
Simu hizo ni Nokia Lumia 530, Nokia Lumia 630 na Nokia Lumia 930 ambazo mfumo huo unawapa watumiaji na wataalamu wa masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) kujitengenezea bidhaa mbalimbali kupitia Window Phone 8.1. 
Meneja wa bidhaa wa Microsoft, Kingori Gitahi aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa simu hizo.
Alisema kupitia bidhaa hizo mtumiaji atakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi kutumia huduma za mawasiliano ya moja kwa moja kwa njia ya simu  kama Skype na zile za Microsoft Office hasa katika masuala ya biashara.
Aliongeza kuwa simu hizo zina uwezo wa kutumia laini mbili kama wateja wengi wanavyopenda na kwamba watumiaji wa simu za mkononi za Tigo, Airtel na Vodacom watapata muda wa maongezi wa bure na vifurushi vya mtandao.

No comments: