MBIO ZA MWENGE KUZINDUA MIRADI 72 MKOANI MWANZA


Miradi 72 ya maendeleo ya Sh bil. 23 inatarajiwa kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru, utakaokimbizwa kwa siku nane mkoani hapa, ambao utapokelewa leo kutoka mkoa wa Simiyu.
Hayo yalielezwa jana na Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Evarist Ndikilo wakati akitoa taarifa ya mwenge huo, iliyosomwa kwa niaba yake na Mratibu wa Mbio za mwenge mkoani hapa, Diana Rwechungura.
Alisema thamani hiyo inatokana na michango ya wananchi inayofikia zaidi ya Sh bil. 2.9, Serikali Kuu Sh bil. 9.5, michango ya halmashauri Sh bil. 2.3 na michango ya wahisani Sh bil. 8.1.
Alisema miradi itakayozinduliwa katika mbio za Mwenge ni ya sekta za afya, kilimo, ufugaji, maji na hifadhi ya mazingira.
Alisema ujumbe wa mwaka huu wa Mwenge huo unasema ‘Katiba ni sheria kuu ya nchi, jitokeze kupiga kura ya maoni tupate Katiba mpya’, ambao utaandamana na kaulimbiu za kudumu za mapambano dhidi ya Ukimwi, rushwa, malaria na vita dhidi ya dawa za kulevya.

No comments: