Baadhi
ya wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), wametaka kuongezwa kwa
huduma za malipo ya nauli na posho kwa wanachama wanaokwenda kwenye matibabu ya
rufaa nje ya vituo vyao, sambamba na kugharamia upimaji wa vinasaba (DNA).
Walisema
hayo walipozungumza wakati wa kikao cha pamoja baina ya wanachama wa mfuko huo
katika kijiji cha Mwamgongo, Kigoma Vijijini mkoani hapa na viongozi wa mkoa wa
mfuko huo.
Walisema
kuwa ni vizuri wanachama wanaokwenda kupata matibabu ya rufaa, wagharamiwe nauli na posho na mfuko huo.
Nassib
Ally, mtumishi katika Kituo cha Afya cha Mwamgongo, alisema licha ya sasa
malipo ya nauli na posho za safari kulipwa na mwajiri, lakini wakati mwingine
malipo hayo hayalipwi kwa wakati.
Alisema
hali hiyo huwafanya wanachama kuhangaika kufuatilia matibabu ya rufaa nje ya
vituo vyao vya kazi.
Mussa
Boniface, mwalimu wa Shule ya Msingi Mwamgongo, alitaka mfuko kugharamia huduma
za upimaji wa DNA na kugharamia huduma za matibabu ya nje ya nchi kwa wanachama
wake.
Akizungumzia
maombi hayo, Meneja wa NHIF mkoa wa Kigoma, Elius Odhiambo alisema kwa sasa
mfuko haugharamii malipo ya posho na nauli kwa wanachama wake, wanaokwenda
rufaa nje ya vituo vya kazi. Alieleza kwamba suala hilo litabaki kuwa juu ya
mwajiri.
Odhiambo
alisema kitendo cha kugharamia posho na nauli kwa wanachama, itawalazimu
wanachama hao kuchangia zaidi.
Alieleza
kwamba suala hilo linahitaji mjadala mrefu ambao utaridhiwa na wanachama wote
kuweza kutekeleza hilo.
Meneja
huyo pia alisema suala la maombi ya mfuko kugharamia matibabu ya nje ya nchi,
litabaki chini ya wizara ya afya huku upimaji wa vinasaba ukiendelea kuwa
gharama za mtu binafsi.
No comments:
Post a Comment