HOSPITALI YA APOLLO KUFUNGUA TAWI LAKE DAR OKTOBA



Hospitali ya upasuaji wa moyo ya Apollo iliyopo India, inatarajia kufungua  tawi lake Jijini Dar es Salaam mwezi ujao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, daktari mwakilishi kutokea hospitali hiyo, Hari Prasad alisema kuwa lengo la ufunguzi wa hospitali hiyo ni kusogeza huduma za hospitali hiyo karibu zaidi na wananchi.
Alisema Watanzania wengi wamekuwa wakienda kuzifuata huduma za hospitali hiyo nchini India ambapo wamekuwa wakilazimika kuingia gharama kubwa.
Alisema gharama za usafiri wa ndege, maradhi na nyinginezo zimekuwa ni kikwazo pia kwa Watanzania wa hali ya chini kujipatia huduma hiyo.
"Huduma zitakuwa zikitolewa hapa Dar es Salaam na kuna eneo maalumu ambapo ujenzi utaanza na lengo ni kuwasaidia wananchi wa kawaida kujipatia huduma za afya kwa ukaribu zaidi," alisema daktari huyo wa Hospitali ya Apollo yenye uzoefu wa miaka 31 katika upasuaji wa moyo.
Alisema kuwa itashughulikia magonjwa ya saratani, kisukari na magonjwa yanahusu matatizo ya figo.

No comments: