KAMPUNI ZA SIMU ZATAKIWA KUPELEKA WATUMISHI VYUONI



Kampuni za simu zimeagizwa kupeleka watumishi wake katika vyuo vya mawasiliano, kuwezesha utoaji wa huduma bora.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa alitoa mwito wakati akifungua mkutano wa 48 wa Taasisi ya Afrika ya Kuendeleza Mawasiliano (Afralti).
Profesa Mbarawa alisema teknolojia imekuwa ikibadilika na kukua kwa kasi, hivyo ni muhimu kwa wadhibiti kuhakikisha wateja wananufaika na teknolojia ya mawasiliano.
"Kwa jinsi soko lilivyo kuna umuhimu wa kutoa huduma kwa thamani ya juu, hii itasaidia sana kuleta maendeleo kwa kasi zaidi kwani bila mawasiliano ni vigumu maendeleo kuja kwa kasi," alisema Profesa Mbarawa.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Afralti, Erwin Mwapasa, alisema taasisi hiyo imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali, kuhakikisha teknolojia ya mawasiliano inatolewa katika kiwango cha juu katika nchi za Afrika.
Alisema teknolojia ya habari na mawasiliano kwa sasa imekuwa ni muhimu kwa maisha ya kila siku na imekuwa ikichangia katika maendeleo ya kiuchumi.

No comments: