Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi imesema tuhuma za rushwa zinazoambatanishwa na kazi
ya usaili wa nafasi ya Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji ni hisia tu za wahusika.
Taarifa
iliyotolewa na Msemaji wa wizara hiyo, Isaac Nantanga, inasema tuhuma za kuwapo
kwa rushwa wakati wa kazi ya usaili ni hisia na hazina ushahidi na kuwa usaili
ulifanywa kwa kufuata kanuni na sheria zinazosimamia ajira za watumishi wa
umma.
“
Katika Uwanja wa Taifa ambao usaili ulikuwa ukifanyika kulikuwa na maofisa
mbalimbali kutoka taasisi za wizara hiyo waliokuwa na kazi ya kuhakikisha kazi
hiyo inafanyika kwa usalama.”
Alisema,
nafasi za Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji zilitangazwa katika magazeti na Tovuti
ya Wizara na Idara ya Uhamiaji kufuatana na taratibu Serikali zinazosimamia
ujazaji wa nafasi za kazi katika utumishi wa umma kwa lengo la kuiweka wazi kwa
umma.
Nantanga
alisema waombaji zaidi ya 20,000 walitumia haki yao ya msingi kuomba nafasi
hizo na kutokana na wingi huo, Wizara ilifanya mchujo wa awali na kubakiwa na
maombi 10,500 ya watu wenye sifa.
“Wizara
ilitambua haki ya kila muombaji ya kupatiwa nafasi ya kushindania nafasi hizo,
ikabidi ufanyike utaratibu wa kutafuta eneo lenye nafasi ya kutosha.
“
Nia ya Wizara haikuwa kuleta usumbufu kwa mtu yeyote ila kutoa nafasi sawa kwa
walioleta maombi kushindania nafasi zilizotangazwa,” alisema na kuongeza kuwa
wingi wa watu ni matokeo ya kidemokrasia ya kutoa nafasi kwa kila raia
kushindania nafasi za ajira zinazotolewa.
Akizungumzia
baadhi ya changamoto walizozibaini, Natanga alisema ni kwa baadhi ya waombaji
kufika katika eneo la usaili akiwa mikono mitupu bila kuwa na vifaa vya kawaida
vya kushiriki usaili kama kalamu.
No comments:
Post a Comment