Hospitali
ya Sinza katika Manispaa ya Kinondoni inakabiliwa na msongamano
mkubwa unaodaiwa kuchangia kuzorota utoaji wa huduma kwa wagonjwa.
Diwani
wa Kata ya Sinza, Renatus Pamba alitoa taarifa hiyo wakati wa kikao cha Baraza
la Madiwani la manispaa hiyo.
Kwa
mujibu wa diwani huyo, hivi sasa hospitali hiyo inapokea watu kuanzia 1,500 kwa
siku tofauti na awali ambapo idadi ya wagonjwa ilikuwa takribani 200.
"Hivi
sasa Hospitali ya Sinza imekuwa kama kimbilio la watu mbalimbali wanaohitaji
matibabu hatua inayoifanya ielemewe tunaomba msaada wa dharura mahali pale
ikiwemo ya kuongeza watoa huduma," alisema Pamba.
Aidha
akipokea msaada wa vifaa mbalimbali vilivyokabidhiwa na uongozi wa Redio ya 'E
fm' juzi, Mganga wa zamu wa hospitali hiyo, Dk Ally Njama alikiri
hospitali hiyo kulemewa wingi wa wagonjwa.
"Tunawaomba
watu wenye mapenzi mema kujitokeza kwa ajili ya kutupa misaada ili tuweze
kuboresha huduma za hospitali yetu," alisema Dk Njama.
Alisema
huduma zinazotolewa hapo ni kwa ajili ya wananchi mbalimbali hivyo ni muhimu
kila mtu akajiona kuwa na jukumu la kujitoa katika suala zima la kutoa msaada.
No comments:
Post a Comment