Benki
ya Barclays nchini imezindua mfumo mpya wa utoaji huduma za kibenki nchini bila
kutumia karatasi au kujaza fomu.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kitengo
cha Wateja Binafsi, Kumaran Pather alisema wanajivunia kuwa benki ya kwanza
nchini kutumia mfumo wa utoaji wa huduma za kibenki kwa mfumo huo mpya.
Alisema
kwamba mfumo huo wa kutoa huduma za benki bila kujaza fomu au karatasi ni moja
tu ya huduma mbalimbali ambazo benki hiyo inaleta katika kuboresha huduma zake
kwa wateja.
“Mfumo
huu wa utoaji huduma za kibenki bila kutumia karatasi unachukua nafasi ya
matumizi ya karatasi katika kupata huduma ikiwemo fomu mbalimbali za kutolea na
kuchukulia pesa,” alisema.
Pather
aliendelea kufafanua, “Uvumbuzi huu ni wa kisasa na tunajivunia kwa sababu
wateja wetu sasa hivi wanatumia chini ya dakika tatu kuweza kukamilisha miamala
yao ikiwemo kulipwa fedha taslimu, kuweka cheki, kutoa pesa na kubadili hundi
kuwa pesa taslimu.”
Aliongeza
kuwa uvumbuzi huo umesaidia kupunguza gharama kwa kiasi kikubwa katika
kuhudumia wateja na pia unapunguza muda wa utoaji wa huduma kwa wateja.
Kwa
upande wake, Meneja Miradi wa Barclays, Jane Mbwilo alisema benki hiyo
inakuwa ya kwanza kutumia mfumo huu nchini na kuwa benki ya kwanza kutumia
mfumo wa kupitisha hundi kwa mitambo inayojiendesha.
“Tumepiga
hatua kubwa sana katika kuboresha huduma kwa wateja wetu na mfumo huu mpya wa
kutoa huduma bila karatasi, wateja wetu wote wanaweza kutumia mfumo huu katika
matawi yote ya Barclays nchini,”
alisema.
Aliongeza
kuwa mkakati wa benki hiyo ni kutumia teknolojia ambayo itasaidia kurahisisha
huduma kwa wateja pia na kupunguza gharama za uendeshaji wa benki.
No comments:
Post a Comment