Kampuni
binafsi za kitanzania zimetakiwa kuwekeza katika ujenzi wa Mji Mpya wa
Kigamboni.
Mwito
huo ulitolewa bungeni jana na Naibu Waziri wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, George Simbachawene wakati akijibu swali la Mbunge wa
Temeke, Abbas Mtemvu (CCM).
Katika
swali lake Mtemvu alitaka kujua Wizara hiyo imewashirikishaje wawekezaji wa
ndani ikiwemo mifuko ya hifadhi za jamii na kampuni za kitanzania.
Simbachawene
alisema mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano na sekta binafsi.
“Serikali
imedhamiria kujenga Mji Mpya wa Kigamboni ili kuwa mji wa kisasa ambao utakuwa
kitovu cha kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii,” alisema.
Alisema
baadhi ya mashirika ya kiserikali kama Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),
Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) yameanza utekelezaji wa awamu ya kwanza ya
mradi mpya wa Kigamboni kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi wa nyumba za
makazi na biashara ndani ya eneo la mradi.
“Mwaka
2007 Serikali iliandaa Mpango Kabambe wa kuendeleza Mji Mpya wa Kigamboni kwa
mujibu wa Sheria ya Mipango Miji na Sheria ya Utwaaji Ardhi.
“Mpango
huu umeainisha maeneo ya matumizi makubwa ya ardhi ikiwemo viwanda, makazi,
taasisi za elimu, biashara, utalii na miundombinu,” alisema Simbachawene.
Alisema
katika mwaka 2013/14 Serikali imeunda Wakala wa Uendelezaji wa Mji Mpya
Kigamboni (KDA) kwa lengo la kusimamia na kuratibu uendelezaji wa Mji wa
Kigamboni.
No comments:
Post a Comment