Treni ya abiria
ya Reli ya Kati, inatarajiwa kuanza safari zake Jumanne Juni 3 mwaka huu, baada
ya kukamilika kwa ukarabati wa stesheni
za Kilosa mkoani Morogoro na Gulwe mkoani Dodoma.
Uongozi wa
Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), umetangaza kuanza kwa usafiri huo jana, baada
ya kusitisha usafiri huo tangu Januari 10, 2014.
Mkurugenzi Mtendaji, Kipallo Kisamfu, katika taarifa yake
iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari, aliwataka wananchi wanatumia usafiri
huo, wafike katika stesheni zilizo karibu yao tangu jana, kukata tikezi za
safari zao.
“Muda wa kuondoka treni kwa siku za Jumanne na
Ijumaa kutoka Stesheni ya Dar es Salaam
kwenda Kigoma na Mwanza, utakuwa saa 11 jioni na zile za kutoka Kigoma
na Mwanza kuja Dar es Salaam katika siku za Alhamisi na Jumapili, ni saa 11
jioni kutokea Kigoma na saa 12 Magharibi kutokea Mwanza,” alisema.
No comments:
Post a Comment