Serikali
mkoani Shinyanga imeanza mikakati ya kujenga hospitali ya
rufaa ya mkoa , itakayogharimu jumla ya Sh bilioni 89 .6.
Lengo
la ujenzi huo ni kupunguza msongamano
wa wagonjwa katika hospitali na
kuwafanya wananchi wasisafiri
umbali mrefu kutafuta matibabu.
Hospitali
hiyo itajengwa katika eneo lenye hekta
53, sawa na ekari 135 katika kijiji cha Negezi Kata ya Mwawaza.
Eneo
hilo ndilo lililopendekezwa tangu awali na kufanyiwa utafiti, ambapo wamiliki
wa maeneo haya wamekwishalipwa fidia zilizotengwa za jumla ya Sh milioni 98.
Hayo
yalisemwa na Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga, Ally Rufunga
mbele ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa.
Alieleza
kuwa fedha hizo ni za mipango ya
kuendeleza majengo na vitendea kazi. Alisema katika bajeti ya mwaka
2012/13 zilitengwa jumla ya Sh bilioni moja.
Alisema
licha ya ujenzi huo kuanza, changamoto
kubwa ni uhaba wa maji. Alisema
Mamlaka ya Maji na Mazingira katika Manispaa ya Shinyanga (SHUWASA), imeahidi kupeleka maji na kwamba
zinahitajika Sh milioni 1.64 kupeleka maji.
No comments:
Post a Comment