Wafanyabiashara wakubwa
wanadaiwa kuwatumia baadhi ya wabunge kuhakikisha muswada wa kufuta misamaha ya
kodi haupelekwi bungeni.
Tuhuma hizo
zilitolewa jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu ya
Serikali (PAC), Zitto Kabwe alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana
baada ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh
kuwasilisha taarifa yake.
Zitto alisema kuna
baadhi ya wafanyabiashara wakubwa wamekuwa wakishirikiana na wabunge kukwamisha
kuletwa kwa muswada huo.
Alisema baadhi ya
wabunge hao wamekuwa wakishirikiana na wafanyabiashara wakubwa wakiwemo wa
makampuni ya uchimbaji wa madini kuwakwamisha.
Kwa mujibu wa Zitto,
endapo muswada huo utafika bungeni na kuwekwa kuwa sheria wafanyabiashara hao
watafutiwa kodi hivyo wamekuwa wakiogopa.
“Ndugu zangu
tusaidieni kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakishirikiana na baadhi ya
wabunge kufanya hili,’’ alisema.
Aidha mwenyekiti huyo
alisema pia Songas imekuwa ikidaiwa kwa muda mrefu lakini haitaki kulipa deni
lake ambalo limekuwa likizidi kuongezeka.
Alisema Songas
wamekuwa wakilalamika kuwa nao wanaidai Shirika la Umeme Tanesco.
“Hawa watu wamekopa
fedha serikalini zaidi ya bilioni 238 lakini sasa hawataki kurejesha na hizi ni
pesa nyingi ni lazima zirudi serikalini,’’ alisisitiza.
Pia Mwenyekiti
huyo alitaka serikali kutumia mashine za kodi, EFDs katika malipo
yake jambo ambalo litasaidia kuokoa fedha nyingi.
No comments:
Post a Comment