Mtu mmoja amekufa na wengine watatu
wameokolewa baada ya mtumbwi waliokuwa wakiutumia kupinduka katika Mto
Kilombero mkoani Morogoro.
Mtumbwi huo uliokuwa na watu wanne,
wawili wakiwa wavushaji waliokuwa
wakivusha shehena ya magunia ya mpunga kutoka upande wa pili wa mto katika
Wilaya ya Ulanga.
Ajali hiyo ilitokea juzi saa 12 jioni
katika kivuko cha Mto Kilombero ukiwa na watu hao na magunia 11 ya mpunga
katika mtumbwi yakisafirishwa ili kufikishwa mjini Ifakara.
Mmoja wa wavushaji katika mtumbwi huo
ambaye amenusurika kifo, Juma Magumbila alisema aliyekufa ni mwenzake
anayeshirikiana katika uvushaji, Rajabu Lipindi ‘maarufu kwa jina la Kidilu’.
Alisema siku hiyo walipata kazi za kuvusha magunia 15 ya mpunga kutoka Wilaya ya Ulanga na walipakia katika mtumbwi huo magunia 11 na kuanza safari ya kuvuka Mto Kilombero.
Alisema siku hiyo walipata kazi za kuvusha magunia 15 ya mpunga kutoka Wilaya ya Ulanga na walipakia katika mtumbwi huo magunia 11 na kuanza safari ya kuvuka Mto Kilombero.
Hata hivyo alisema wakati wakikaribia
kufika upande wa pili, ghafla dhoruba kali ilitokea na
marehemu aliamua kupiga simu kuomba
msaada, na alipokuwa akiendelea kuwasiliana ndipo mtumbwi ulipopinduka
baada ya kupigwa na wimbi kubwa la maji.
Alisema watu wawili
waliokuwemo katika mtumbwi wao walikuwa ni wabeba mizigo wa mpunga ambapo
majina yao hakuyafahamu.
Mkuu wa Wilaya ya Ulanga, Francis Miti,
ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kilombero
akiwa Mjini Mahenge amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusababisha
kifo cha mtu mmoja na wengine watatu kuokolewa.
Mkuu wa Mkoa, Joel Bendera akiwa mjini
Ifakara, Mei 5, mwaka huu, alifahamishwa kuanzia Februari hadi mwanzoni mwa Mei
mwaka huu kuwa watu 11, walifariki dunia kwa nyakati tofauti
baadhi yao kusombwa na maji na wengine kuliwa na mamba waliotapakaa kando ya m
to Kilombero.
No comments:
Post a Comment