Kampuni ya ndege
ya Fastjet itaanza kushirikiana kibiashara na kampuni ya Expedia Group, ambayo
ni kubwa zaidi duniani kwa usafirishaji, masoko na utalii kwa njia ya mtandao.
Hayo yamesemwa
na Makamu wa Rais wa Utalii na Usafirishaji wa Expedia Group, Greg Schulze, alipozungumza na waandishi wa
habari.
Alisema kuwa
Fastjet itafikiwa na mamilioni ya wasafiri kupitia kwenye mtandao wa Expedia
group. Alisema pia Fastjet kwa kupitia Expedia, ambayo ni mmoja wa wakala
wakubwa zaidi kwa usafirishaji kwa mtandao, itaweza kuunganishwa na kampuni
nyingine za mtandao, kama vile Hotwire na Egencia, ambayo ni kampuni ya tano
kwa ukubwa katika huduma ya usafirishaji kwa mtandao, na itakuwa na uwezo wa
kufikia nchi zaidi ya 60 duniani kote.
“Tuna furaha
kupata nafasi hii ya kupanua uwigo wa biashara yetu, tuna imani Fastjet sasa
itafikiwa na mamilioni ya watu kwa njia ya mtandoa, na pia tutaweza kuifanya Fastjet
kufika sehemu kubwa zaidi ya Afrika,” alisema Schulze.
Mkuu wa Biashara
wa Fastjet, Ellis Cain-Jones alisema upatina huo na Expedia group, utawezesha
kupanua zaidi biashara yao ya usafirishaji na pia itaweza kufikia malengo na
mipango yao ya kuwa moja ya kampuni kubwa ya usafirishaji wa njia ya anga.
“Awali, tuliwekeza kwenye kuongeza utumiaji
mtandao wa intaneti katika ukataji wa tiketi ndani ya Afrika, pili mkakati wetu
ni kupanua biashara katika soko la kimataifa.
Kutumia Expedia
group kutaifanya Fastjet kulifikia kiurahisi zaidi soko la kimataifa.
Tumehamasika mno kufanya kazi na Expedia group,” alisema Cain-Jones.
No comments:
Post a Comment