Benki ya Afrika
(BOA) Tanzania, imetoa ofa ya miezi sita ya pugunzo la riba ya mikopo ya nyumba
kutoka asilimia 18 hadi asilimia 16,
ili kuwezesha wananchi wengi kumiliki nyumba.
Meneja
Mwandamizi wa Masoko wa benki hiyo, Solomon Haule, alisema jana jijini Dar es
Salaam kuwa ofa ya punguzo la riba,
inalenga kuwezesha wananchi kumiliki nyumba.
“Ofa hii imeanza
Mei, mwaka huu na itadumu kwa miezi sita,” alisema na kuongeza kuwa punguzo hilo ni kubwa ikilinganishwa na hali
halisi, lakini benki imeamua kufanya hivyo
ili kuwezesha Watanzania wengi kumiliki nyumba za kuishi au biashara kwa
kuwa masuala hayo ni ya msingi kwa ustawi wa jamii.
Licha ya punguzo
hilo, benki imeongeza muda wa kulipa mkopo kutoka miaka 15 hadi miaka 20 ambayo
inatoa fursa kwa watu wengi kuitumia.
Alihamasisha
watu wengi hasa vijana kujitokeza na kuitumia fursa hiyo, na kufafanua kuwa
anayestahili kupata mkopo ni mwenye
mshahara au kipato cha Sh milioni 1.4 kwa mwezi au watu wawili wanaoshirikiana
kutaka kumiliki nyumba kama baba na mama, ambao watakuwa na pato la pamoja la
Sh milioni 2 kwa mwezi.
Akitoa mfano
alisema mkopo huo utawawezesha wananchi kununua nyumba za bei rahisi
zinazojengwa na mashirika hapa nchini yakiwemo Shirika la Taifa la Nyumba
(HNC), Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) na Mfuko wa Mafao wa Watumishi wa Umma
(PSPF).
“Siyo kwenye
mashirika hayo tu, bali hata ukiona nyumba inauzwa na mtu binafsi pia tumia
fursa hii kumiliki nyumba,” alisema Solomon.
Akifafanua zaidi
alisema ili kupata mkopo huo, mteja atatakiwa kuwa na asilimia 10 na benki
itampatia mkopo wa asilimia 90 kwa nyumba mpya na asilimia 20 kwa nyumba
iliyotumika.
No comments:
Post a Comment