Mbunge wa Ubungo,
John Mnyika ametoa Sh milioni 10
kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Malamba Mawili iliyopo Kata ya
Msigani katika Manispaa Kinondoni.
Akizungumza na baadhi ya wananchi wa eneo hilo juzi,
walioongozwa na Mwenyekiti wao wa Mtaa, Bakari Said (CCM), Mnyika alisema fedha
hizo,zinazotolewa kupitia Mfuko wa Mbunge zitaingizwa katika akaunti ya mtaa
huokabla ya Juni 30, mwaka huu.
Zahanati hiyo inajengwa kwa ushirikiano wa wananchi wa eneo
hilo kwa uchangiaji wa vifaa mbalimbali vya ujenzi, ikiwemo saruji, mabati,
nondo, fedha na matofali.
Alisema lengo la fedha hizo ni kuunga mkono nguvu za
wananchi wa eneo hiloili kuhakikisha ujenzi huo unakamilika haraka, hivyo
kuondoaadha ya wananchi hao kutembea umbali mrefu kwa ajili ya kutafuta
matibabu.
Awali, akitoa taarifa fupi kwa Mnyika, Said alisema
makadirio yao ujenzi wa zahanati yanaonesha kuwa Sh milioni 45
zitatumika hadi ujenzi utakapokamilika.
Said alisema hatua ya wananchi wa eneo hilo, kuunganisha
nguvu za ujenzi wazahanati hiyo, kumetokana kuchoshwa na adha ya kwenda umbali
mrefukutafuta huduma za afya.
No comments:
Post a Comment