Wafanyakazi
wa Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (Tazara), wamesisitiza msimamo wao wa
kuendelea kugoma kutoa huduma, hadi hapo watakapohakikishiwa kwamba malimbikizo
ya mishahara yao yatalipwa na malipo ya miezi ijayo, yatafanyika.
Mwenyekiti
wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli (Trawu), Kanda ya Dar es Salaam, Yusuph
Mandai, alisema jana Dar e s Salaam kwamba wafanyakazi wa shirika hilo
hawatorudisha huduma kama ilivyotarajiwa hadi watakapolipwa madai yao.
Akifafanua
zaidi, alisema mshahara wa Februari ambao unatakiwa kulipwa na Serikali ya
Tanzania unafikia Sh milioni 140 na mpaka Aprili ni Sh bilioni 1.5.
“Tulipwe
kwanza ndio turudishe huduma…na pia ni vyema tuhakikishiwe mshahara kwa
miezi inayokuja,” alisema Mandai mbele ya wafanyakazi hao ambapo pia aliuliaza
aliye tayari kurudi kazini anyooshe kidole ambapo hakuona hata mmoja aliyefanya
hivyo.
Mandai
alipouliza wafanyakazi hao, walio tayari kuendelea na mgomo hadi hapo
watakapolipwa waonyooshe vidole kusisitiza suala hilo, wote wakafanya hivyo.
Akizungumzia
suala hilo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk Shaban Mwinjaka, alisema
fedha kwa ajili ya mishahara ya wafanyakazi hao ziko kwenye mchakato.
“Mimi
hapa (Dk. Mwinjaka) ndio natoka Hazina kufuatilia suala hilo…hadi saa sita
mchana fedha zilikuwa bado kuingizwa…ila tunafuatilia kwa kina hadi
zipatikane,” alisema Dk Mwinjaka.
Juzi
akizungumzia suala hilo, Dk Mwinjaka alisema Serikali ya Tanzania imekubali
kutoa mshahara wa Aprili na Februari, huku Serikali ya Zambia ikishughulikia
mshahara wa Machi na Mei.
Katika
hatua nyingine hali za abiria wa usafiri huo zilikuwa za kukatisha tamaa jana
ambapo wengi walikuwa wamesambaa bila kujua hatma ya huduma hiyo kwao.
Elizabeth
Shaban aliyekuwa akisafiri kwenda Ifakara, Morogoro alisema haelewi utatuzi wa
suala hilo kwani wanawasikia viongozi wa wafanyakazi hao wakiwaambia wasafiri
endeleeni kusubiria.
No comments:
Post a Comment