Serikali
imesema iko katika hatua za mwisho za kukamilisha mfumo wa teknolojia ya
ufungaji wa vifaa vya ulinzi vijulikanavyo kama CCTV kwa miji mikubwa nchini
ikianzia na Jiji la Dar es Salaam.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe aliliambia Bunge jana wakati akijibu
swali la nyongeza la Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM).
Chikawe
alisema wizara yake iko katika hatua za mwisho za kukamilisha mfumo huo ambao
kwa kuanzia, utafanyiwa majaribio katika Jiji la Dar es Salaam na kisha
kusambazwa miji mingine mikubwa.
“Mheshimiwa
Naibu Spika, ni kweli kuwa Serikali iko katika hatua za mwisho za kuweka vifaa
maalumu vya ulinzi katika maeneo mbalimbali ya umma nchini.
“Kwa
kuanzia, hivi karibuni tutafunga mfumo huo katika Jiji la Dar es Salaam na
kisha kusambazwa katika miji mingine mikubwa kwa kuanzia Zanzibar, Mwanza,
Mbeya, Dodoma, Arusha,” alisema Chikawe.
Alisema
utaratibu huo ni wa kawaida sana duniani katika kudhibiti uhalifu na akatolea
mfano wa Marekani, ambako kuna msemo kuwa big brother is watching, ukirejea
mfumo huo uliowekwa kila mahali.
Katika
swali lake la msingi, Lugola alitaka kufahamu kuna sababu gani za msingi kwa
Serikali kutofunga vifaa vya kisasa ili kuzuia na kudhibiti uhalifu katika miji
mikubwa ya Dar es Salaam, Mwanza, Moshi, Morogoro na Mbeya.
Akijibu
swali hilo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereirra Ame Silima alisema
Closed Circuit Television (CCTV) ni muhimu katika kupunguza uhalifu wa aina
mbalimbali katika miji nchini.
Alisema
kwa kutambua hilo, Jeshi la Polisi katika Programu ya Maboresho inatekeleza
jukumu lake la msingi la ulinzi kwa kuwa na miradi 27 ya ICT ukiwemo wa
kufuatilia taarifa za usalama barabarani.
“Hata
hivyo, ufanisi wa jukumu hili unakwamishwa na ufinyu wa bajeti,” Silima
aliliambia Bunge.
Alisema
ufungaji wa vifaa hivyo ni jambo mtambuka linaloshirikisha wadau mbalimbali
wakiwemo Wizara ya Ujenzi, Mipango Miji, Serikali za Mitaa na watu binafsi.
“Huu
ni mradi mkubwa unaohitaji utafiti wa kutosha wa kimuundo, kisheria na
rasilimali fedha. Wizara yangu ni mshauri na msimamizi wa kazi za mradi huu
katika kudhibiti uhalifu,” alisema Naibu Waziri.
Alisema
Serikali inaendelea kufanya uchambuzi wa mapendekezo ya kibiashara na sekta
binafsi ili kuwekeza teknolojia hii na miundombinu yake katika kutimiza malengo
ya usalama wa nchi.
No comments:
Post a Comment