Bodi
ya Huduma za Maktaba Tanzania (Bohumata) imesema mahitaji ya taarifa
yanayotolewa kwa njia ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) kwa jamii
yameongezeka maradufu hali inayowafanya washindwe kutoa huduma nzuri.
Aidha,
Bodi hiyo inashindwa kugharimia huduma hizo kutokana na uwezo wa kifedha kuwa
mdogo.
Mkuu
wa Kitengo cha Mipango wa Bohumata, Comfort Komba alisema hayo jana
alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Alisema
pamoja na kuwepo kwa ukosefu wa fedha zipo juhudi za kuendelea kutoa huduma ya
TEHAMA katika vituo vingine.
“Kwa
sasa huduma hii ipo katika Maktaba ya hapa Dar es Salaam lakini tunajitahidi
kupeleka katika vituo vingine ili kuiwezesha jamii kushiriki kikamilifu katika
mipango ya maendeleo ya nchi kwa kupata taarifa sahihi na kwa wakati,” alisema
Komba.
Akifafanua
kuhusu mfumo wa Tehama, Komba alisema ni katalogi ya kielektroniki inayowezesha
kutoa mchango mkubwa katika kusaidia juhudi za serikali za kuelimisha jamii kwa
kupatikana kwa habari kutoka katika vitabu, magazeti, ramani na picha kwa
haraka zaidi.
“Mfumo
huu una uwezo wa kutunza kumbukumbu nyingi kwa kutumia nafasi ndogo katika
maktaba kwani habari huwa katika mfumo wa kielektroniki, pia unahamasisha
matumizi ya kielektroniki, kuhabarishana na kuhamasisha matumizi ya habari kwa
jamii,” alisema.
Alisema
kwa sasa Chuo cha Ukutubi na Uhifadhi wa Nyaraka (Slads) cha Bagamoyo kimeongeza
udahili wa wanafunzi mpaka kufikia 1,093. Alisema idadi hiyo imekuwa
kubwa kutokana na kuwepo kwa uhitaji mkubwa wa wanataaluma wa ukutubi na
uhifadhi nyaraka kwenye shule za serikali na za watu binafsi, vyuo, taasisi na
ofisi mbalimbali nchini.
No comments:
Post a Comment