Serikali
imesema iko imara katika kuendelea na kusimamia juhudi zinazofanywa na Benki ya
Afrika katika kuinua mitaji kupitia mpango wa sita wa kukuza mitaji wa benki
hiyo (GCI-VI).
Kauli
hiyo imetolewa na Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum alipokuwa akihutubia
magavana wa nchi za Afrika katika mkutano wa mwaka wa wadau wa Benki ya
Afrika jijini Kigali, Rwanda.
Alisema
kuwa kupitia mpango wa GCI-VI, Tanzania imekuwa na uwezo wa kulipa hisa zake
zipatazo Dola za Marekani 2,683,429.52 katika awamu ya tatu kwa muda
uliopangwa.
Alisema
kupitia mpango huo, Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika kulipa hisa
zake zipatazo Dola za Marekani 2,683,429.52 katika awamu ya tatu kwa muda
uliopangwa.
Aidha,
Saada alimpongeza Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, Dk Donald
Kaberuka na uongozi mzima kwa kusimamia na kuongoza kwa umahiri mkubwa majukumu
waliyonayo ya kibenki na kuhakikisha inasonga mbele daima na kuifanya kuwa
benki bora barani humu.
Rais
wa Rwanda, Paul Kagame akifungua mkutano huo, alisema ili kufikia uchumi
wa kati katika Afrika kwa miaka 50 ijayo, inabidi nguvu kubwa
ielekezwe kwenye sekta binafsi ambayo itatengeneza ajira kwa vijana na
wanawake.
Mkutano
huo ni wa siku tano kuanzia 19 hadi 23 Mei mwaka huu. Kabla ya ufunguzi,
mkutano huu ulitanguliwa na mikutano mbalimbali ya Magavana ambao ni Mawaziri
wa Fedha kutoka nchi mbalimbali barani Afrika, wakifuatana na wajumbe
kuwakilisha nchi zao.
No comments:
Post a Comment