Mabasi
yaendayo mikoani yanalipa Sh 65,000 kwa ajili ya kupuliza dawa ndani ya magari
hayo ikiwa ni hatua ya kupambana na ugonjwa wa dengue nchini. Imeelezwa.
Hatua
hiyo imetokana na makubaliano ya wamiliki wa mabasi hayo na Mamlaka ya Udhibiti
wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) kudhibiti ugonjwa huo kuenea katika
mikoa mingine yanakofanya safari zake.
Naibu
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Stephen Kebwe alisema hayo jana akijibu
swali la nyongeza la Mbunge wa Kinondoni, Iddi Azzan (CCM) aliyetaka kujua kwa
nini upulizaji wa dawa katika mabasi, unatozwa gharama kubwa na mikakati ya
dharura kukabiliana na ugonjwa huo.
Dk
Kebwe alisema malipo hayo ni makubaliano ya wamiliki wa magari, kutokana na
uzalendo wa nchi na kukabiliana na ugonjwa huo, hivyo hakuna mmiliki
anayeshindwa kulipa fedha hizo.
Alisema
mipango ya dharura, kukabiliana na ugonjwa huo ni pamoja na kuvipatia vitendea
kazi vituo vyote vya afya nchini, kuweza kubaini maambukizi ya ugonjwa huo.
Alisema
pia vipo vipimo vingine vinatarajia kuwasili nchini kupitia Bohari ya Madawa
nchini (MSD) na vitaongeza upatikanaji wake pale vinapohitajika.
No comments:
Post a Comment