Serikali
kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imetenga kiasi cha Sh bilioni 3
katika bajeti ya fedha ya mwaka 2014/15 kwa ajili ya huduma za uzazi wa mpango.
Hayo
yalielezwa jana na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Kebwe S. Kebwe
wakati akizindua upya kampeni ya Nyota ya Kijani kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa,
iliyofanyika jana kwenye Uwanja wa Michezo wa Nyamagana.
Alisema
Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa
Linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA), wametoa Sh bilioni 6.4 ikiwa ni pamoja
na vifaa ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha matumizi ya huduma ya uzazi wa mpango.
Alisema
kiwango cha utumiaji wa uzazi wa mpango kipo juu katika nchi zilizoendelea,
ambapo ni asilimia 72.4.
Alisema
Tanzania kiwango cha utumiaji, bado kipo chini, ikiwa ni asilimia 27 hivyo
Watanzania wanapaswa kwenda sambamba na maelekezo ya dunia ili wasipitwe na
wakati.
Kufuatia
hali hiyo, Naibu Waziri huyo alitoa wito kwa wadau wote, kuungana pamoja katika
kuongeza kasi ya upatikanaji na utumiaji wa huduma za uzazi wa mpango.
Alisema
imani potofu imechangia utekelezaji wa huduma za uzazi wa mpango kwenda
polepole, hasa kwa upande wa wanaume ambao ushiriki wao umekuwa mdogo kwa
kuhofia nguvu za kiume kupungua, imani ambayo siyo ya kweli.
“Tumemuona
ndugu yetu Mayunga ametoa ushuhuda wake mbele yetu hajazungumzia nguvu za kiume
kumpungua tangu afanyiwe, ushuhuda
uliotolewa
ni elimu tosha kuliko kwenye majukwaa,” alisema Naibu Waziri Kebwe.
Alisema
ukosefu wa uzazi wa mpango katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, unachangia kurudisha
nyuma takwimu za kitaifa, ambapo kwa sasa ni asilimia 12 wakati Kanda ya
Kaskazini inafikia asilimia 50.
Alisema
uzinduzi mpya wa kampeni ya Nyota ya Kijani, yenye kaulimbiu ya ‘Fuata nyota ya
kijani upate mafanikio’ ni njia pekee ya kuondokana na imani potofu miongoni
mwa jamii.
Alisema
Mkoa wa Mwanza una vituo 363 vinavyotoa huduma za afya za mama na mtoto,
vikiwemo vituo 72 vinavyotoa huduma ya uzazi wa mpango.
Alisema
uzinduzi unaofanyika, utakuwa chachu ya mabadiliko na ari mpya katika kuboresha
huduma za uzazi wa mpango ikiwa ni
pamoja
na upatikanaji wa dawa za uzazi wa mpango za kutosha na kwa wakati na
kupiga
vita na kuondoa dhana potofu kuhusu njia za kisasa za uzazi wa mpango.
No comments:
Post a Comment