Rais
Jakaya Kikwete, amemteua Gabriel Nderumaki, kuwa Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya
Magazeti ya Serikali (TSN), wachapishaji wa magazeti ya Habari Leo, Habari Leo
Jumapili, Spoti Leo, Daily News na Sunday News.
Taarifa
iliyotumwa jana kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu, na
kusainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, uteuzi huo umeanza Mei
19, 2014.
Kabla
ya uteuzi huo, Nderumaki alikuwa Kaimu Mhariri Mtendaji wa Kampuni hiyo tangu
Desemba 2012. Nafasi zingine alizowahi kushika ni pamoja na Mhariri wa Michezo,
Mwandishi Mkuu, Mhariri wa Habari na Mhariri wa Biashara wa gazeti la
Daily News.
Nderumaki
ambaye amekuwa katika fani ya habari tangu 1994, ana Shahada ya Uzamili ya
Mawasiliano ya Umma kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine aliyoipata mwaka
2013.
Pia
ana Shahada ya kwanza Uhusiano wa Umma na Matangazo kutoka Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam, Stashahada ya Juu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kwa Umma
kutoka iliyokuwa Shule ya Habari (TSJ) na Cheti cha Ualimu kutoka Chuo cha
Ualimu Kinampanda, Singida.
Nderumaki
pia amewahi kuhudhuria mafunzo ya mwaka mmoja ya kijeshi katika Kambi ya
Msange, Tabora na kuhudhuria mafunzo mbalimbali ndani na nje ya nchi.
No comments:
Post a Comment