Kanisa
la Tanzania Assemblies of God (Victory Christian Center Terbenacle) Mbezi A
jijini Dar es Salaam linaloongozwa na Mchungaji Kiongozi, Dk Huruma Nkone,
katika kuelekea maadhimisho ya miaka 75 ya Tag, limeandaa ibada maalumu ya
Uamsho.
Ibada
hiyo itaongozwa na Mhubiri maarufu duniani, Rais wa SOS Mission International,
Mwinjilisti Johannes Amritizer kutoka Sweden na inatarajia kutikisa Jiji la Dar
es Salaam na vitongoji vyake, Mei 11, mwaka huu.
Mwinjilisti
Amritizer ni miongoni mwa wahubiri wakubwa duniani ambaye Mungu amempa vipawa
vya ajabu hususani katika maeneo ya ishara na miujiza kwa watu ambao wana
mahitaji mbalimbali kama vile magonjwa na matatizo mengine ambapo pia
Mwinjilisti huyu amekuwa akifanya makongamano makubwa sehemu mbalimbali duniani
pamoja na kujikita vyema katika kulichambua vyema Neno la Mungu.
Akizungumza,
Dk Nkone alisema hiyo ni fursa ya kipekee na wanajisikia kuheshimiwa kwa
mhubiri mkubwa mwenye ratiba nyingi duniani kukubali kuja Tanzania kuendesha
ibada maalumu.
Akieleza
zaidi, alisema tayari maandalizi ya ibada hiyo yamekamilika na tayari kanisa
limejipanga kuhakikisha maelfu ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wanahudhuria
ibada hiyo ya kipekee ambayo haijawahi kutokea ambapo mabasi maalumu kutoka
Mwenge yameandaliwa kuwabeba washiriki wote.
No comments:
Post a Comment