IPTL WAJIWEKA SAWA KUUZA UMEME SENTI 6 KWA UNITI



Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), imepanga kushusha bei ya umeme kwa Shirika la Umeme (Tanesco), kutoka kati ya senti za kimarekani 26 mpaka 30 kwa uniti moja, mpaka senti sita na nane.
Chanzo cha habari za uhakika kutoka Wizara ya Nishati na Madini, kilieleza jana kuwa hatua hiyo, imetishia kupoteza soko kwa kampuni za kigeni zinazozalisha umeme na kuuza kwa bei ya juu nchini. 
Kwa sasa, kampuni zingine katika soko zinatoza kati ya senti za Kimarekani 38 na 60 kwa kila uniti.
Kampuni ya PAP iliyonunua IPTL katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa jijini Dar es Salaam jana, imesema Watanzania watafurahia gharama hizo za chini baada ya  utekelezaji wa mkakati wao wa utanuzi na ubadilishaji wa mfumo wa mitambo yao, ambao utaongeza uwezo wa uzalishaji wa umeme  kutoka megawati 100 za sasa mpaka megawati 500.
Taarifa fupi iliyotolewa jana na Katibu na Mshauri wa Masuala ya Sheria wa IPTL/PAP, Joseph Makandege, imesema ikiwa kampuni ya ufuaji umeme, wanaelewa faida za kiuchumi zitokanazo na umeme wa gharama nafuu kwa mteja mmoja mmoja na kwa maendeleo ya kiuchumi ya nchi nzima. 

No comments: