Shirika
la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limesema linatarajia kurudisha wahamiaji
haramu 115 walioingia nchini kutokea Ethiopia mwishoni mwa wiki ijayo.
Ofisa
Mwendeshaji wa Taifa wa shirika hilo, Charles Mkude, alisema hayo juzi
jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari.
Alisema
wamefanya hivyo kupitia mikakati miwili iliyowekwa na serikali ya Japan na
Marekani kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa
Kimataifa.
Kwa
mujibu wa Mkude, mwaka 2013, zaidi ya wahamiaji 160,000 waliingia nchini
na Afrika Kusini kupitia Kaskazini mwa Saud Arabia.
Alisema
wameamua kusaidia wahamiaji hao kurudi nchini kwao kwa kushirikiana na serikali
zao.
‘’
Wafanyakazi wote wa IOM, Uhamiaji, maofisa wa Magereza na maofisa kutoka
Ethiopia nao watashiriki kusaidia katika safari yao, ’’alisema Mkude.
Aliongeza
kuwa wahamiaji waliokamatwa walifungwa katika magereza mbalimbali yakiwemo ya
Pwani, Iringa, Mbeya, Morogoro na Tanga.
Aidha,
kati ya watu 220 walikamatwa wakiwa wadogo, hivyo IOM itawasaidia masuala
yote ya usafiri kwani hawana taarifa zozote za kusafiri.
‘’Tumehamasika
kuwasaidia kwani watu hawa wanaishi katika mazingira hatari kwakuwa
hawajui kuongea Kiswahili na hawana ndugu yeyote hapa nchini, pia
Serikali haina pesa za kutosha kuwasafirisha’’ aliongeza.
Awali
, alisema kwa kipindi kirefu Tanzania imekuwa na ongezeko la wahamiaji
haramu kutoka pembe ya Afrika hasa Ethiopia na Somalia kutokana na matatizo ya
vita ya wenyewe kwa wenyewe.
No comments:
Post a Comment