Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadik amekanusha tuhuma zilizoandikwa
na gazeti moja la kila siku (si HabariLeo) kuwa Mkuu wa Wilaya ya
Temeke Sophia Mjema ametishiwa maisha baada ya kuvunja danguro la Temeke.
Akizungumza
ofisini kwake jana, Mkuu huyo wa Mkoa alisema gazeti hilo liliandika habari
hiyo ambayo si ya kweli na kuongeza kuwa ina lengo la kudidimiza operesheni
hiyo.
“Naomba
niwatoe hofu habari hizo si za kweli na Mkuu wa Wilaya Sophia Mjema ametueleza
kuwa si kweli na hivyo tunaamini mwandishi wa habari hiyo hana lengo zuri,”
alisema Sadik.
Aliongeza
kuwa danguro hilo lilikuwa ni kichaka cha wanawake wadogo wanaojihusisha na
ngono, wavuta bangi na dawa za kulevya.
“Kwa
kweli kama kuna madanguro mengine tunaomba yafichuliwe ili wanaofanya biashara
hizo waweze kuchukuliwa hatua za kisheria haraka na tunaahidi kuwa operesheni
hii itakuwa endelevu,” alisema.
Aidha
alitoa rai kwa wananchi ambao katika mitaa wanayoishi kuna madanguro watoe
taarifa hizo haraka kwa vyombo vya usalama ili hatua zichukuliwe mara
moja.
No comments:
Post a Comment