Wanafunzi
wa Darasa la Saba waliofanya mtihani wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) wakiwa
darasa la sita, watafanya mtihani mwingine wa aina hiyo kabla ya kufanya
mtihani wa mwisho wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu kwa lengo la
kuongeza ufaulu.
Kaimu
Mkurugenzi wa Elimu ya Msingi, Sarah Mlaki alisema hayo jana wakati akielezea
mikakati ya Programu ya BRN katika elimu ya msingi kuongeza ufaulu na
kupunguza wanafunzi wanaomaliza elimu ya msingi bila kujua kusoma na kuandika.
Alisema
awali wanafunzi hao walifanya mtihani katika muhula wa pili kwa masomo ya
Hisabati Kiswahili na Kiingereza Novemba mwaka jana na sasa watafanya tena
awamu ya pili ili kumudu masomo yao vizuri .
Alisema
ingawa kuna changamoto ya ukosefu wa fedha katika kutunga mtihani wa BRN
lakini mtihani huo unatarajia kufanyika mapema iwezekanavyo.
Alisema
katika mtihani wa sasa wataangalia iwapo wanafunzi wameelewa yale ambayo
yalionekana katika mtihani wa kwanza ikiwa ni pamoja na mada ambazo walifeli
sana na walimu kupewa mbinu za ufundishaji.
Alisema
katika kukabiliana na hali hiyo, wameandaa miongozo ya masomo ya Hisabati,
Kiswahili na Kiingereza na itakamilika Julai mwaka huu, kutoa mafunzo kwa
wawezeshaji 18 wa ngazi ya Taifa kwa ajili ya kuwafundisha walimu mahiri wa
masomo hayo katika ngazi ya Halmashauri.
“Tumefanya
uteuzi wa walimu 600 mahiri wa masomo hayo ambao ni 15 toka kila halmashauri
kwa halmashauri zote 40 ambao watawafundisha walimu wa shule za msingi kwa
mwaka wa fedha ujao,” alisema.
Mlaki
alisema pia wataendesha mitihani ya majaribio ili kuwabaini wnafunzi wenye
mahitaji ya ziada katika kujifunza, kufanya uchambuzi wa maswali yenye
changamoto kwa wanafunzi kuelewa na walimu katika kujifunza na kutoa mafunzo ya
ziada kwa wanafunzi hao.
No comments:
Post a Comment