Hatima
ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu kwa
mujibu wa sheria, iko mikononi mwa waziri mwenye dhamana.
Kauli
hiyo imetolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati akihitimisha michango
iliyotolewa na wabunge kabla ya bajeti ya mwaka 2014/15 ya ofisi yake
kupitishwa juzi.
Pinda
alisema kwa mujibu wa sheria, umepangwa utaratibu ni wakati gani uchaguzi huo
ufanyike kwa kuhesabu miaka mitano tangu uchaguzi uliopita ulipofanyika ambao
unaangukia Oktoba mwaka huu.
“Lakini
sheria hiyo hiyo inampa mamlaka waziri mwenye dhamana kuweza kuahirisha hizo
tarehe akiona zipo sababu za kuweza kufanya hivyo,” alisema.
Aliendelea
kusema kwamba ikifika wakati ikaonekana iko haja ya kuahirisha tarehe ya
uchaguzi huo, watashauriana na Rais na wadau wengine waone namna ya
kufanya.
No comments:
Post a Comment