Tume
ya Kikristo ya Huduma za Jamii (CSSC), imeomba Serikali kutumia dola kusambaratisha
mtandao wa ugaidi, ambao umekuwa ukilipua makanisa na maeneo yake.
Katika
tamko hilo, Tume hiyo ilitaja tukio la
wiki iliyopita, ambapo bomu lililipuka katika hosteli iliyo katika eneo la
Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), inayomilikiwa na kanisa hilo na kujeruhi
mhudumu.
Akizungumza
jana katika eneo kulipolipuka bomu hilo, Mwenyekiti wa Tume hiyo, Kanda ya Ziwa Askofu Benson Bagonza, alisema Serikali inayo nguvu ya kutosha
kuangamiza mtandao huo.
Alisema
mtandao huo umekuwa ukikosesha amani kutokana na matukio ya kigaidi
yanayofanywa na baadhi ya watu kwa kupigwa na mabomu, kumwagiwa tindikali
pamoja na makanisa kuchomwa moto.
“Tamko
letu haliko kwa ajili ya kumtuhumu mtu yeyote kuhusika na tukio hili na sisi
kama Watanzania tuendelee kuwa kitu kimoja,” alisema.
Alitaka
Serikali isikubali kuendelea kuchezewa na mipaka ya nchi iwe salama kwa ulinzi
kwani yaweza kuwa waliofanya tukio hilo ni watu wa ndani ya nchi au nje ya
nchi, ili uhuru wa kukusanyika na kuabudu uwepo bila kujali itikadi za kidini.
Askofu
Irene Nzwalla wa Kanisa la Hossana Mwanza alisema kupitia maombi Mungu
atamfichua mhusika wa tukio hilo, ikiwa waumini watashirikiana katika maombi,
kwani tukio hilo sio la Kanisa la KKKT pekee, bali ni la Wakristo
wote.
Hata
hivyo Askofu wa KKKT, Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria, Andrew Gulla
alisema hali ya majeruhi Bernadetha Alfred ambaye amelazwa katika Hospitali ya
Rufaa ya Bugando inaendelea vizuri baada ya
kufanyiwa
upasuaji.
No comments:
Post a Comment