Kampuni
ya simu za mikononi ya Tigo Tanzania, imezindua huduma mpya ya kutuma na
kupokea fedha kwa njia rahisi na ya ufanisi zaidi kwa wateja wenye simu zenye
programu aina ya android na iOS, ambayo ni huduma ya kwanza ya aina hiyo Afrika
Mashariki.
Mkuu
wa Huduma za kifedha wa Tigo, Andrew Hodgson alisema Dar es Salaam jana kuwa
kuanzia sasa watumiaji wa simu za kisasa za smartphones nchini, wataweza
kufanya miamala yoyote ya Tigo Pesa, ikiwemo kulipia huduma na bidhaa.
“Unaweza
kutuma fedha kupitia benki, na kuongeza salio kwa uharaka na urahisi zaidi kwa
kutumia ‘Tigo Pesa Application’, unaweza ukaona namba zote za simu
zilizohifadhiwa katika simu yako wakati wa kuchagua kutuma fedha kupitia huduma
hii ya ‘Tigo Pesa App’,” alisema Hodgson.
Alisema
pia mtumiaji wa simu hizo anaweza kuhifadhi kumbukumbu za malipo yake pamoja na
miamala ya kibenki aliyoifanya kwa ajili ya kuipata kiurahisi kama itahitajika
maelezo yake siku za karibuni.
Hodgson
alisema katika huduma hiyo, mteja ataweza kupata huduma ya Tigo Pesa
katika mtandao wa Tigo bila kuingia gharama yoyote ya data, na kwamba wataweza
kutumia akaunti zao za Tigo Pesa popote pale walipo duniani kupitia intaneti ya
Wi-Fi au mtandao wowote uliopo wa intaneti kupitia simu kama amesajiliwa na
Tigo Pesa.
Wiki
mbili zilizopita, Tigo ilitoa huduma ya Facebook bure kwa wateja wake, jambo
linaloelezwa na Hodgson kuwa ni moja ya utekelezaji wa dira ya kampuni ya Tigo
katika kuendeleza ubunifu na huduma ambazo ni rahisi kutumia na
zinazowafurahisha wateja wake.
No comments:
Post a Comment