Mkoa wa Dodoma umetenga Sh milioni 500
katika bajeti yake ya Mkoa kwa mwaka ujao wa fedha, kwa ajili ya kutoa motisha
kwa shule, waalimu na wanafunzi watakaofanya vizuri katika mitihani ya kuhitimu
elimu ya msingi na sekondari.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Rehema
Nchimbi alisema hayo katika Uwanja wa Jamhuri mjini hapa katika salamu zake za
makaribisho kwenye Maonesho ya Wiki ya Elimu.
Alisema hayo mbele ya Waziri Mkuu,
Mizengo Pinda, aliyekuwa mgeni rasmi.
Aliishukuru Serikali kupitia Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa (Tamisemi) kwa kuupa heshima kubwa Mkoa wa Dodoma kuwa mwenyeji wa
maonesho hayo kitaifa.
Alitaja
maendeleo mazuri yaliyofikiwa kielimu mkoani hapa tangu kuzinduliwa kwa
Mpango wa Taifa wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) kuwa ni waalimu wengi
kujiendeleza kielimu kutoka daraja moja kwenda jingine la juu kitaaluma, na
baadhi yao kujiunga na Chuo Kikuu Huria
cha Tanzania (OUT), wakisoma huku wakiwa kazini.
Alisema Mkoa huo umefanya marekebisho
kwenye baadhi ya sera zake za ndani ili kuendana na Mpango wa Matokea Makubwa
Sasa ili kujenga mazingira rafiki ya
kutoa matokea ya elimu kwa haraka.
Alieleza kuwa ofisi yake, imefanya makubaliano
na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ili mahafali yajayo ya wahitimu wake,
yafanyike kitaifa Dodoma ili Mkoa uweze kutoa tuzo za wahitimu wa kozi za
Ualimu, watakaohitimu kutoka chuo hicho na pia yawe yakifanyika rasmi mkoani
hapa.
No comments:
Post a Comment