Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu
(CDA) imeendesha zoezi la kubomoa nyumba eneo la Mlimwa Kusini,
karibu na yalipo majengo ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika Manispaa ya
Dodoma.
Kwa mujibu wa Msemaji wa CDA, Anjela
Msimbila wameendesha zoezi hilo juzi baada ya notisi za kuhama za siku 90
kumalizika. Alisema kwamba uvunjaji huo, ulifanyika kwa amani huku wengine
wakiwasaidia.
Alisema watu waliobomolewa nyumba
zao, walishapewa viwanja. Takribani nyumba 65 zilibomolewa ili kupisha ujenzi
wa barabara eneo hilo.
Pamoja na Msemaji wa CDA kusema
kwamba kazi hiyo ilifanyika kwa mujibu wa sheria, baadhi ya wakazi walisema
kwamba wameshtushwa na sasa hawana makazi.
Inaaminika kwamba watu 150
wameathiriwa na shughuli hiyo ya bomoa bomoa.
Wakazi hao walisema wanasikitishwa
na kitendo cha kushtukizwa na kubomolewa, huku wengi wao wakiwa hawajatoa vitu
vyao ndani na vibaka wakitumia nafasi hiyo, kukwapua vitu vya watu kwa
visingizio vya kusalimisha vitu vya watu ambao hawakuwepo nyumbani wakati huo.
Mmoja wa mabalozi wa nyumba kumi, ambaye hakutaka jina lake
liandikwe, alisema anasikitishwa na tukio hilo, linalowarudisha katika
umasikini wananchi waliosota kwa muda mrefu kutafuta kwa kujinyima na
kufanikiwa kupata vitu hivyo, japo ni vichache kwa ajili ya familia zao.
Alisema uvunjaji huo, ulikosa utu,
kwani wabomoaji hawakuweza kuacha hata nyumba moja walioikuta, ikiwa haina
mtu na kutoa mfano wa nyumba iliyokuwa na watoto 5 wanaoishi peke yao na
huku wazazi wao wakiwa safarini, ilivyovunjwa na kuwaacha watoto hao
wakihangaika.
Mwananchi Mwingine,
aliyejitambulisha kwa jina moja la Mgoile, alisema nyumba 65 zilizobomolewa,
zina watu zaidi ya 150 kutokana na nyumba moja kuishi familia tatu mpaka tano
na wote hawana makazi, kutokana na zoezi hilo la kushtukizwa.
Mtu huyo alihoji kwanini Mwenyekiti wao, asiitishe mkutano na kuwajulisha watu wote ili waondoe vitu vyao.
‘’Hawa watu wana uelewa sana, ona hamna fujo wala malalamiko yoyote katika zoezi zima, hivi kweli kama huyu mama Mwenyekiti angetuita kwenye mkutano na kutuambia, tungeacha kuhamisha vitu na kubomoa wenyewe ili kuondoa mbao na bati?’’ Alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa huo, Zubeda Haji alisema yeye hawezi kuzuia maendeleo yanapokuja na kwamba nyumba hizo zote zilizobomolewa, tayari wamiliki wake walishapewa viwanja vingine, wakajenge ili kupisha barabara inayotarajiwa kujengwa baadaye.
Mtu huyo alihoji kwanini Mwenyekiti wao, asiitishe mkutano na kuwajulisha watu wote ili waondoe vitu vyao.
‘’Hawa watu wana uelewa sana, ona hamna fujo wala malalamiko yoyote katika zoezi zima, hivi kweli kama huyu mama Mwenyekiti angetuita kwenye mkutano na kutuambia, tungeacha kuhamisha vitu na kubomoa wenyewe ili kuondoa mbao na bati?’’ Alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa huo, Zubeda Haji alisema yeye hawezi kuzuia maendeleo yanapokuja na kwamba nyumba hizo zote zilizobomolewa, tayari wamiliki wake walishapewa viwanja vingine, wakajenge ili kupisha barabara inayotarajiwa kujengwa baadaye.
No comments:
Post a Comment