Watu watano wamekufa maji
baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama ndani ya Ziwa Victoria.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa
wa Kagera, George Mayunga alisema ajali hiyo ilitokea Mei 23 mwaka huu saa 8
usiku.
Boti ya Mv Kitoko II
waliyokuwa wakisafiria kutoka Bugombe kupitia Kasenye kwenda Mganza wilayani
Chato, ilizimika ghafla ikiwa katikati ya ziwa.
Alisema boti hiyo
inayomilikiwa na Mama Chacha aishiye Muganza , ilikuwa na abiria hao watano,
ambao wote walikufa maji.
Maiti aliyepatikana ni
mfanyabiashara raia wa Rwanda, Jane Mlekatete (36) ambaye mwili wake ulikutwa
ukielea.
Wengine waliozama
ambao hawajapatikana ni Chikola Filbert (22) mkazi wa Muganza, Mapinduzi Daud (
38 )mkazi wa Mwanza, Asha na Suzy waliotambuliwa kwa jina moja moja, wote
wakazi wa Kasenyi na Mavombe (23) ambaye ni mkazi wa Muganza.
Alisema chanzo cha
ajali hiyo ni boti kubeba mzigo mkubwa. Kwa mujibu wa Kamanda, ilikuwa imebeba
magunia 210.
Chanzo kingine cha ajali
hiyo ni kwamba licha ya kubeba mzigo mkubwa, ilisafiri usiku wakati
kukiwa na upepo mkali na mawimbi yaliyosababisha injini ya boti hiyo kuzimika
kabla ya kuzama.
No comments:
Post a Comment