Soko la Kariakoo
jijini Dar es Salaam limepongezwa kwa kukuza uchumi nchini, kutokana na kupokea
wafanyabiashara kutoka ndani na nje ya nchi.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya FNB Tanzania, Dave Aitken
alisema hayo Dar es Salaam jana wakati akizindua tawi jipya la benki
hiyo.
Alisema ingawa
ni wachangiaji ipo haja ya taasisi za
fedha kuwafikia wajasiriamali wengi.
Alisema
wafanyabiashara wengi wa soko hilo wana mikakati mikubwa ya kuvutia bidhaa zao,
jambo linalosababisha wafanyabiashara kutoka nchi zisizokuwa na bahari kufika
na kujipatia bidhaa.
Kariakoo ni eneo
ambalo wanafika wafanyabiashara kutoka nchi zisizokuwa na bahari, ambapo
kutokana na shughuli za biashara, husaidia kukuza uchumi wa nchi.
Kuhusu tawi hilo, alisema lengo la benki hiyo ni kuwa
mstari wa mbele katika kukuza sekta za fedha, kwani ina mpango wa kuleta wataalamu kutoka Ukanda
wa Jangwa la Sahara katika sekta ya kilimo na madini, ambao watakuwa chachu ya
ukuaji wa uchumi wa nchi.
Kwa upande wake,
Mtendaji Mkuu, Andy Watkins, alisema uchumi wa Tanzania umekuwa kwa asilimia 7,
ukilinganisha na miaka iliyopita.
Alisema ongezeko
hilo, limetokana na shughuli mbalimbali, kama vile uchimbaji wa madini, utalii,
viwanda na kilimo.
Alisema Kariakoo
ni kitovu cha biashara, ambapo waingizaji na wasambazaji hutumia soko hilo,
kufanya biashara zao, hivyo huduma za kibenki zitaimarisha maendeleo yao katika
ngazi ya mtu mmoja mmoja.
No comments:
Post a Comment