Mwenyekiti
wa Makampuni ya IPP amewataka wasomi nchini kuacha kubagua kazi badala yake
wafungue macho na kuziona fursa zilizopo katika maeneo yao ili waweze
kujiajiri.
Alisema
iwapo vijana watafungua macho na kuona fursa zilizopo, nusu ya tatizo la ajira
nchini litapungua kwa kuwa vijana watakuwa wanazitumia fursa hizo kujiajiri na
kuajiriwa pia.
"Tatizo
la vijana wetu wanachagua kazi, kwa usomi wao wanajiona hawawezi kufanya kazi
fulani…wavulana hawataki kufanya kazi zingine kwa kudhani ni za wanawake na
wanawake pia wanaona baadhi ya kazi ni za wanaume," alisema Mengi.
Alisema
hayo wakati wa kutoa zawadi kwa tweet bora ya mwezi Aprili.
Mengi
alisema fikra na mawazo ya vijana juu ya kazi ni lazima yabadilike ili macho
yao yafunguliwe waone fursa nyingi zilizopo nchini.
Mengi
pia alisema wazazi wanalo jukumu la kuwaandaa watoto wao namna ya kujitegemea,
ikiwa ni pamoja na kumtanguliza Mungu na kuwa waaminifu katika shughuli zao.
Swali
la tweet la Aprili lilihoji namna gani wazazi wanapaswa kuwaandaa watoto wao
ili wawe na uchumi mzuri, mawazo mengi yaliyotolewa waliacha kumtegemea Mungu na kuwa mwaminifu
maishani.
Mshindi
wa kwanza katika shindano hilo ni Abnery Mwogela ambaye ni mwalimu wa shule ya
msingi kutoka Njombe aliyejinyakulia Sh 1,000,000. Mshindi wa pili
aliyejinyakulia Sh 500,000 ni Samson Shila na mshindi wa tatu aliyepata Sh
300,000 ni Gerald Nyaissa wa Dar es Salaam.
Wazo
la mshindi wa kwanza lilisema mzazi amuandae mwanawe kuishi kwa kujiamini,
kuthubutu, kuanza kufanya anachodhani ni vyema akifanye kwa wakati huo cha
kiuchumi, wazo la mshindi wa pili lilisema mzazi amwandae mtoto katika mambo makuu
manne, elimu, kupenda kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na kupenda kumcha Mungu.
Wazo
lililoshinda nafasi ya tatu lilisema kila siku mzazi amnong'oneze mwanawe,
Mungu amewapa matajiri saa 24 kwa siku sawa na anayokupa wewe, yatumie masaa
hayo kwa faida."
No comments:
Post a Comment